Januari 27 - Februari 2, 2010
 
Toleo Na. 118
   Maoni ya Mhariri
Kugawanya majimbo sawa lakini...
TUME ya Uchaguzi (NEC) imetanganza kwamba halmashauri zenye mapendekezo ya kugawanywa kwa majimbo ya uchaguzi ziyapeleke ili ifikapo Februari 28 mwaka huu yawe yamefika. Tangazo hili la NEC linatokana na sababu kwamba sasa Tume imepata vigezo vipya itakavyovitumia katika kugawanya majimbo ambavyo ni pamoja na mawasiliano, idadi ya watu, jiografia, uwezo wa kubeba wa Ukumbi wa Bunge na mipaka...
Sitta na Lowassa wagongana tena

Kamati ya Mwinyi yawashindwa
Ujasusi watumika kuwinda vigogo wa CCJ
KIWEWE cha kuanzishwa kwa Chama Cha Jamii (CCJ) kinachohusishwa na baadhi ya vigogo maarufu ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinashika kasi huku kamati ya wazee iliyoongozwa na rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, ikishindwa kumaliza makundi kama ilivyokusudiwa...
 Makala

Karume azidi kuota mbawa
WAKATI kuahirishwa ghafla kwa kikao cha Kamati Kuu ya CCM na vikao vya Halmashauri Kuu ya chama hicho kukihusishwa na mitafuruku ya kisiasa Zanzibar...
 Rai ya Jenerali

Viongozi wa wilaya wachaguliwe
Jenerali Ulimwengu
MSINGI wa rai ninayoitetea hadi sasa katika mfululizo wa makala zangu ni kwamba tunapaswa kuangalia upya utaratibu tuliouzoea wa uongozi, na tufanye maamuzi muhimu kuhusiana nao...
 Makala

Prof Mwakyusa awaponza watumishi Mbeya
Felix Mwakyembe
HOFU imetanda kwa baadhi ya wafanyakazi wa Hospitali ya Wilaya ya Kyela waliotoa kero zao kwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Prof David Mwakyusa alipotembelea hospitali hiyo...
 
 
free counter

counters

 
 Makala   Makala   Makala   Makala
Viongozi Arusha sasa wahofu kumwalika Kikwete
VIONGOZI wa serikali mkoani Arusha wanadaiwa kuingia hofu ya kumwalika tena mkoani hapa Rais Jakaya Kikwete kufuatia tukio la wiki iliyopita la Rais Kikwete kugoma kukabidhi gari la msaada ya kubeba wagonjwa...
Jeshi la Polisi Arusha ndani ya kashfa nzito
JESHI la Polisi mkoani Arusha limeingia katika kashfa kubwa baada ya askari wake wawili kuhusishwa na tuhuma za kushiriki vitendo vya ujambazi na uporaji wa kutumia silaha...

 

Wanapambana na masikini badala ya umasikini!
Gululi Kashinde
UNAPOZUNGUMZA wanyonge pengine unaweza kupata maana nyingi na pana zaidi kadri ya uelewa wa neno lenyewe. Lakini kwa upande wangu ninamaanisha masikini wenye kipato cha chini...
Viongozi: Kashfa zinapoandama Taifa, jitambulisheni na wanyonge msalimike
Joseph Mihangwa
NENO mapinduzi linaweza kutafsiriwa kumaanisha mabadiliko ya ghafla kwa njia ya matumizi ya nguvu ya kiwango fulani, ili kubadili hali fulani ya mambo, kutoka hali iliyokithiri kwa ubaya...
Maridhiano ya Zanzibar yatokane na kanuni
Lula wa Ndali-Mwananzela
KWANZA sina budi kushukuru barua pepe nyingi ambazo nimezipata kutoka kwa Wazanzibari wengi. Karibu barua zote nilizopata madai makubwa matatu yanatolewa...

 

Wasomi na uchambuzi butu
Godfrey Dilunga
WIKI hii kumeibuka mjadala kuhusu kuanzishwa kwa kile kinachoelezwa chama kipya cha siasa chenye kuhusishwa na baadhi ya vigogo ndani ya CCM, ambao baadhi wamekwishakanusha kuhusishwa nacho...
Nimetimiza ombi lenu!
Privatus Karugendo
NINAANDIKA makala hii kuwafahamisha wasomaji wangu kwamba hatimaye nimetimiza ombi lao. Nimekuwa nikipokea ujumbe mfupi wa simu za mkononi na barua pepe, nikiombwa kuandika kitabu kutokana na makala zangu au maoni yangu mengine...
'Elimu ya bure', michango kibao!
Chesi Mpilipili
KATIKA juhudi zake za kuhakikisha kuwa kila mtoto wa Kitanzania anapata elimu, Serikali ilipunguza kwa kiasi kikubwa ada ya wanafunzi wa shule za sekondari ambapo wazazi walitakiwa kulipa Shilingi 20,000 tu...

 

Wito Wangu, Imani Yangu: Maandiko ya padri mwenye ghadhabu
Johnson Mbwambo
INGAWA nilianza kumfahamu Padri Privatus Karugendo katika miaka ya tisini wakati akituandikia makala kwenye gazeti la Rai, zama zile za Habari Corporation, ni majuzi tu nimepata kumwelewa vizuri padri huyu...
TFF ilipaswa kuzishirikisha klabu
Ibrahim Mkamba
KIGEZO kimoja kikubwa cha kujua kwamba mtu anakuheshimu kwa dhati ni kuwepo kwa mawasiliano baina yake na wewe kuhusu jambo lolote ulilo na matashi au maslahi nalo...