UKIPEWA kazi ya nchi, lazima ujiheshimu. Huwezi kupewa kazi ya nchi halafu unaishi kihunihuni. Kazi za uhuni ziko tele. Nenda kafanye uhuni wako kule. Kwa hiyo, nchi zote zina miiko. Hapa kwetu hatuna. Wameiacha miiko ya Azimio la Arusha, hawakuweka miiko mingine. Sasa ni holela tu