
WAKATI joto la ufisadi uliofichuliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, kiasi cha kuibua shinikizo la kutaka baadhi ya viongozi kujiuzulu likiwa halijapoa, uhalali wa mali za viongozi wanane wa kitaifa umezua utata na tayari viongozi hao wamepewa siku 30 kuwasilisha nyaraka ili kuthibitisha umiliki wao, Raia Mwema, limeleezwa.
Viongozi hao wametakiwa kuwasilisha nyaraka zao zikiwamo taarifa za kibenki ndani ya siku hizo 30, kuanzia Mei 21 hadi Juni 19, mwaka huu.
Katibu wa Utumishi wa Sekretariati ya Maadili ya Umma, Tixon Nzunda, amethibitisha taarifa hizo na kwamba, muda huo utakapofika bila viongozi hao kuwasilisha nyaraka zao, watapelekwa katika Baraza la Maadili la Tume hiyo.
Katika maelezo yake kwa mwandishi wetu@
Toa maoni yako